Maandalizi ya awali ya utekelezaji wa mradi wa maji wa Bangulo utakaosimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wenye gharama ya Shilingi Bilioni 40 yameanza rasmi kwa Mkandarasi wa mradi kampuni ya SINOHYDRO kutoka China kuanza hatua ya maandalizi ya kukusanya vifaa vya ujenzi.
Ikiwa ni miezi miwili sasa tangu kusainiwa kwa mkataba wa utekelezaji wa mradi na kukabidhi eneo la ujenzi kwa Mkandarasi, utekelezaji wa mradi huu unalenga kunufaisha wananchi 450,000.
Akielezea hatua mbalimbali zilizofikiwa za utekelezaji wa mradi Meneja wa usimamizi wa mradi kutoka kampuni ya SINOHYDRO ya China Ndugu Xie Zhen amesema kuwa kazi za awali zilizofanyika ni pamoja na utafiti wa udongo kubaini ubora wa udongo sehemu itakayojenga tenki la maji Bangulo pamoja na kituo cha kusukuma maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...