Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa kushirikiana na Taasisi ya Kiharusi Duniani (The World Stroke Organization) imezindua mafunzo maalumu kwa wataalamu wanaoshughulikia magonjwa ya kiharusi kwa lengo la kuendelea kuboresha huduma kwa wagonjwa hao.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya nje (OPD) Dkt. Elimeena Meda amesema mafunzo hayo ni muhimu kwani kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa kiharusi hivyo ni muhimu watoa huduma wote kujua namna bora ya kuwahudumia wagonjwa hao.

“Tumeona sababu ya kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa kiharusi, mafanzo haya yanahusu kada zote zinazoshiriki katika mnyororo wa kuwahudumia wagonjwa wa kiharusi ili kuboresha huduma wanapokuwa hospitalini hadi wanaporuhusiwa” ameongeza Dkt. Meda.

Kwa upande wake, muandaaji wa mafunzo hayo kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Sarah Matuja amebainisha kwamba ugonjwa wa kiharusi umekuwa tishio nchini na unawakumba watu wenye umri wa miaka kati ya miaka 40 hadi 60 na hivyo kuathiri nguvu kazi ya jamii.

Mafunzo hayo yanatolewa na wataalamu bingwa wa magonjwa ya kiharusi duniani kuanzia leo Januari 9 hadi Machi 19, 2024 ambapo yatahusisha wakufunzi ambao ni Madaktari Bingwa wa kiharusi duniani na yatafanyika kwa nadharia na vitendo.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...