#TARURA kutuma wataalamu kufanya usanifu

Mikumi, Kilosa

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inatarajia kuanza usanifu wa daraja la kudumu la chuma (Mabey Bridge) litakalojengwa ili kuunganisha vijiji vya Nyali na Nzumbo katika kata ya Ulaya-Mikumi Wilayani Kilosa.

Hayo yameelezwa na Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff wakati akiongea na wananchi wa kata hiyo kwenye ziara yake ya kikazi ya kukagua hali ya miundombinu wilayani Kilosa.

“Nitawatuma wataalamu wangu wa TARURA Makao Makuu waje wafanye usanifu wa ujenzi wa daraja la kudumu la chuma ili kuunganisha vijiji hivi vya Nyali na Nzumbo”. Alisema

Pamoja na hilo, amemwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro kuanza mara moja ujenzi wa daraja la watembea kwa miguu (Kiteputepu) ili wananchi wa vijiji hivyo waendelee kupata huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Vile vile Mhandisi Seff ameelekeza kufanyika kwa tathimini ya uharibifu wa barabara za Mikumi ili ziwekwe kwenye mpango wa dharura wa kurudisha mawasiliano haraka iwezekanavyo.

Awali, Mbunge wa Jimbo la Mikumi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge - TAMISEMI Mhe. Dennis Londo amesema barabara nyingi za Jimbo la Mikumi zimeharibika vibaya kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na kuiomba TARURA kuangalia uwezekano wa kukarabati hasa barabara za Kivungu-Kilangali Km. 1.5, barabara ya Miyombo-Dodoma Isanga Km. 10 pamoja na ujenzi wa daraja la kudumu la Nyali-Nzumbo.

Daraja la watembea kwa miguu katika mto Nyali ambalo linaunganisha vijiji vya Nyali na Nzumbo litajengwa kufuatia lile la awali kuvunjika.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...