Na. Mwandishi wetu, Arusha - Namanga.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amethibitisha kutokuwepo kwa usafirishaji haramu wa biashara ya binadamu katika mpaka wa Namanga na Kenya hususani kwa watoto na wenye ulemavu. 
 
Mhe. Katambi amethibitisha hayo Januari 3, 2023 Jijini Arusha katika Wilaya ya Longido alipofanya ziara katika mpaka wa namanga kwa ajili ya kukagua hali ya utoaji huduma kwa abiria.

Amesema taarifa ambazo hivi karibuni zimesambazwa katika mitandao ya kijamii juu ya watoto na wenye ulemavu kusafirishwa kinyume na sheria na kupelekwa nchini kenya kwa ajili ya kutumikishwa zipuuzwe kutokana na hali ya ulinzi na usalama uliopo katika mpaka huo.

Ametoa rai kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea kudhibiti vipenyo visivyo halali ikiwa ni pamoja na kuweka polisi jamii ili kuwachukulia hatua watakao bainika wanapita bila kufuata utaratibu
.
Aidha, amesema Serikali ya Mhe, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mfumo  wa kielekroniki wa kupata hati ya kusafiria kwa muda mfupi hivyo hakuna sababu ya kusafiri bila kufuata utaratibu.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...