MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umeungana na wadau wa michezo nchini, kuchangia timu za taifa za Tanzania zinazoshiriki katika mashindano mbalimbali ya kimataifa ikiwemo Taifa Stars, ambayo inashiriki michuano ya AFCON 2023, inayotarajiwa kuanza Januari 13, 2024 nchini Ivory Coast.

Katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya timu hizo, iliyoongozwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, kwenye hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia Januari 11, 2024, PSSSF imenunua kupitia mnada, jezi ya marehemu Joel Bendera kwa shilingi milioni 11.

Marehemu Bendera alikuwa kocha mzalendo wa kikosi cha Taifa Stars kilichoshiriki AFCON kwa mara ya kwanza mwaka 1980.

Pichani, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (kushoto), akikabidhi jezi hiyo, kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhandisi Cyprian Luhemeja (wapili kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba (watatu kushoto) na Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama PSSSF, James Mlowe.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...