Raisa Said,Tanga

MAMLAKA ya vitambulisho vya Taifa 'NIDA' mkoa wa Tanga imezindua zoezi la ugawaji wa vitambulisho  kwa wananchi wapatao  165, 000  ambavyo vitakuwa vikipatikana kupitia ofisi za kata na vitongoji ili kurahisisha upatikanaji kwa walengwa wote.

Akizindua zoezi hilo Mkuu wa mkoa wa Tanga  Waziri Kindamba amemwagiza meneja wa NIDA wa mkoa huo kuhakikisha ifikapo january 31 , 2024 wananchi wote ambao waliomba  wawe tayari wameshapata huku akiwataka wananchi kutoa taarifa kwenye ofisi za wilaya pale ambapo itatokea mtu yoyote kudai pesa ili aweze kupewa kitambulisho chake .

"Kwa mkoa wetu wa Tanga Mamlaka yetu ya NIDA imeweza kusajili wanannchi 1, 191, 488 sawa na asilimia 88,   namba za vitambulisho zilizo zalishwa ni  9, 50 ,392  sawa na asilimia  80 ya wakazi wote wenye umri wa miaka kuanzia 18 na vitambulisho vilivyopokelewa na kusambazwa ni 7,  96, 155 sawa na asilimia 83 ya wananchi wote waliokidhi vigezo  ni matumaini yangu kuwa wananchi wote kupitia wilaya zote mtajitokeza kupata vitambulisho vyenu,  jambo ambalo ni la kusisitiza  ni kwamba vitambulisho hivi vitagawiwa bure kama itatokea mtu yeyote atakudai fedha taarifa hizo zifike mara moja kwenye ofisi za wakuu wa wilaya na hatua kali zichukuliwe mara moja"  alisisitiza Kindamba.

Meneja wa Mamlaka ya vya vitambulisho vya Taifa NIDA  mkoa wa wa Tanga Kitashu Lembira alisema  kuwa  zoezi hilo la ugawaji wa vitambulisho ambalo limezinduliwa na mkuu wa mkoa  leo litafanyika  katika ngazi za wilaya ili kuwarahisishia na kuwawezesha wananchi wote waliokidhi kupata  akipongeza juhudi za serikali kwani  malalamiko ya wananchi kuhusu kukosekana kwa vitambulisho hivyo muda mrefu impshapatiwa ufumbuzi.

"Tumezindua mkoani lakini wakuu wa wilaya kuazia  jumatatu ijayo vitambulisho vyote kuanzia ngazi za wilaya kata vijiji na vitongozi vitakuwa vimeshasambazwa na kutakuwa na majina yamebandikwa kwenye  mbao za matangazo ,  kikubwa ni kuipongeza na kuishukutu serikali hususan kwa awamu hii ya sita kwa mkoa wa Tanga  tunajivunia kwa sababu ni kipindi ambacho changamoto cha kukosekana kwa vitambulisho  inakwenda kuisha na kila mwenye namba ya kitambulisho cha taifa atapata kitambulisho chake" alisema Lembira

Kama alivyotuagiza mkuu wa mkoa kuwagawia vitambulisho ananchi wote wenye namba za NIDAigikapo january 31, 2024  wananchi wote watapata na tutashusha mpaka ngazi vya vijiji na vitongoji  kikubwa tywaombe tu wananchi wawe watulivu kwa sababu tumeweka utaratibu mzuri kwa yule mwananchi ambaye atakqenda na atakosa ktambulisho chake atayoa taarifa kwa mtendaji wa kata ambaye naye atalazimika kufikisha katika ngazi ya wilaya ili kitambulisho kiweze kupatikana" aliongeza 

Wakizungumza baadhi ya wananchi waliopata vitambulisho vyao wakiwemo Waziri Omari na Mwanamisi Mbwana  wameishukuru na kuipongeza  serikali kwani kwa kuwapatia vitambulisho hivyo kumewasaidia kupata huduma mbalimbali ikiwemo za kifedha. 

"Naishukuru sana Serikali kwa kutupatia vitambulisho hivyi tulikuwa tunavisubiri kwa muda mrefu tumekuwa tukikosa baadhi ya huduma ,  kitambulisho cha Taifa  kinahusika maeneo mengi tumekuwa tukikosa huduma"





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...