NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limefanya kikao na wadau wa bidhaa za mabati nchini chenye lengo la kujenga uelewa ili kuweka mikakati mahususi kwa bidhaa za mabati zinazozalishwa na kuingizwa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 17,2024 katika ukumbi wa TBS Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Uaandaji wa Viwango Bw. David Ndibalema ambaye amemuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TBS, amesema kuwa katika kuunga juhudi za serikali TBS inaendelea kuwajibika ili kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini na zile zinazotoka nje ya nchi zinakidhi vigezo vya ubora.

Aidha Bw. Ndibalema ametoa wito kwa wazalishaji wa bidhaa na wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa nje ya nchi kuhakikisha bidhaa hizo zinakidhi Viwango vya ubora ili kuondokana na malalamiko na kulinda thamani ya fedha kwa wateja.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Sheria, Ukaguzi na Ufuatiliaji Dkt,Candida Shirima amesema kuwa TBS inapokuwa ikitekeleza majukumu yake kisheria inautaratibu wa kukutana na wadau wake  ili kukumbushana matakwa ya kisheria katika masuala mbalimbali likiwemo la viwango vya ubora.

Mkutano huo umelenga kugusia masuala mbalimbali kuhusiana na uagizaji wa bidhaa za mabati nchini pamoja usambazaji wa bidhaa hizo ili kuhakikisha bidhaa hizo zinakidhi matakwa ya ubora.
Mkurugenzi wa Uaandaji wa Viwango Bw. David Ndibalema akizungumza katika kikao cha wadau wa bidhaa za mabati nchini kilichofanyika leo Januari 17,2024 kwenye Ofisi za Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Uaandaji wa Viwango Bw. David Ndibalema ambaye amemuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TBS, akifungua kikao cha Wadau wa bidhaa za mabati nchini kilichofanyika leo Januari 17,2024 kwenye Ofisi za Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam
Kaimu Mkurugenzi wa Sheria, Ukaguzi na Ufuatiliaji Dkt,Candida Shirima akizungumza katika kikao cha wadau wa bidhaa za mabati nchini kilichofanyika leo Januari 17,2024 kwenye Ofisi za Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam
Kaimu Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Bw.Francis Mapunda akizungumza katika kikao cha wadau wa bidhaa za mabati nchini kilichofanyika leo Januari 17,2024 kwenye Ofisi za Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam


Baadhi ya wadau wa bidhaa za mabati nchini wakiwa kwenye kikao na TBS kilichofanyika leo Januari 17,2024 kwenye Ofisi za Makao Makuu ya TBS Jijini Dar es Salaam

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...