Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo Januari 25, 2024 amemsindikiza na kumuaga Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar Es Salaam mara baada ya kumaliza Ziara yake nchini Tanzania.

Rais Salvador alikuwa nchini kwa Ziara ya Siku Tatu, pamoja na maeneo mengine alitembekea katika kiwanda cha ‘Tanzania Biotech Products ltd’ (TBPL) na kuzungumza na wafanyakazi ambapo alisisitiza jukumu muhimu la TBPL katika jitihada za kutokomeza Malaria nchini.

Ziara za Viongozi wa Kimataifa kuja Tanzania ni fursa ambazo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuzifungua kwa lengo la kuendeleza ushirikiano baina ya Tanzania na Mataifa mengine Duniani ili kuleta maendeleo nchini.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...