NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

MAGONJWA maarufu ya zamani kwa wazee sasa yanaongezeka kwa vijana ambapo hivi karibuni, utafiti umeonyesha ongezeko la uwiano wa vijana wenye shinikizo la damu lililoongezeka kutoka 0.2% hadi 25.1% katika Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeripoti ongezeko za aina 5 za kisukari aina ya kwanza miongoni mwa watoto na vijana kati ya mwaka 2011 na 2021.

Ameyasema hayo leo Januari 19, 2024 Jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Amesema kuwa wakati maendeleo makubwa yamepatikana, dhahiri katika kupunguza matokeo duni ya lishe kama vile kudumaa kutoka 34.7% katika 2014 hadi 31.8% mwaka 2018, anemia kati ya wanawake wa umri wa uzazi imepungua kutoka 44.8% katika 2015 hadi 28.8% kwa mwaka 2018 pamoja na kupungua kwa maambukizi mapya ya VVU, hata hivyo baadhi ya maeneo ya vijana kama vile afya ya akili bado yanahitaji juhudi zaidi.

Aidha amesema kuwa tunahitaji ushahidi zaidi wa kisayansi ambao unaweza kuchangia kuimarisha utendaji wa sekta yetu ya afya na ushirikiano ulioonyeshwa hapa kwamba kuhusisha wanasayansi mbalimbali na wataalam wa afya ya umma wa ndani na nje ya Tanzania ambao ni mfano wa kuigwa.

"Nimefurahi kuona Taasisi zetu za Serikali kama Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi ya Jamii Muhimbili, Chuo Kikuu cha Dodoma, Halmashauri mbalimbali za Mikoa na Wilaya, Taasisi ya Afya ya Ifakara, Taasisi ya MDH pamoja na ZAPHA+ kutoka Zanzibar zikiwa sehemu ya kazi hii". Ameeleza Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesisitiza juu ya umuhimu wa kuendeleza ajenda ya afya miongoni mwa vijana ili kuboresha afya na ustawi wao kwa ujumla, kuinua kizazi cha afya na watu wenye kinga kali, uwezo wa kufikiri kwa umakini na wenye ubora kitaaluma ambayo itachangia maendeleo ya taifa letu.

"Ninatoa wito kwa kila mmoja wetu, watunga sera, watafiti, watoa huduma za afya, wazazi, wanajamii na vijana kuibebaa ajenda hii. Mafanikio haya hayawezi kupatikana bila kushirikiana na washirika wa ndani na wa kimataifa na wafadhili". Amesema

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH) Bi.Mary Sando amesema kuwa jukumu muhimu katika kuitisha Mtandao wa ARISE unaojumuisha taasisi wanachama 21 kutoka nchi tisa (Botswana, Burkina Faso, Ethiopia, Ghana, Nigeria, Rwanda, Afrika Kusini, Tanzania na Uganda) za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo umekuwepo kwa miaka mingi kutokana na ushirikiano wa ndani na kimataifa na umesaidia kupitisha ruzuku,maombi, na usambazaji na tafsiri ya matokeo ya kisayansi yenye athari katika programu zinazoweza kutekelezeka.

Aidha amesema azma yao katika mkutano huo ni kusudi endelevu la kuziba pengo la utafiti kwa kupitia njia Shirikishi ya mafunzo,kwa lengo la kujenga uwezo na tafsiri ya maarifa.

"AAPH imeendelea kudumisha mashirikiano na vyombo mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya,Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Taasisi za ndani na nje ya nchi kama vile MUHAS, UDOM na HIGH, pamoja na shirika letu dada la MDH, ambapo tunawasaidia katika shughuli za utafiti na kuhakikisha ubora wa data ili kufahamisha ufanyaji maamuzi"Bi.Mary Sando Amesema.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akikabidhiwa tuzo maalumu ya kutambua mchango anaoutoa kwenye sekta ya afya kwa kushirikiana na taasisi zisizo za kiserikali katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH) Bi.Mary Sando katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza jambo na mwakilishi kutoka Chuo Kikuu cha Harvard, Bw. Mark Elliott katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH) Bi.Mary Sando akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Michael Battle akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.







Baadhi ya wadau mbalimbali wakiwa katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika leo Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...