Naibu Waziri wa afya DKT Godwin Mollel amesema kuwa jumla ya asilimia 10 ya wanawake wanaotoa mimba wanafariki kwa utoaji mimba usio salama.

Akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu Conjesta  Rwamlaza lililohoji kuhusu vifo vitokanavyo na utoaji mimba usio salama vina ukubwa na madhara gani naibu waziri alisema kuwa tafiti zilizofanywa matatizo yatokanayo na utoaji wa mimba ni moja ya sababu inayochangia vifo vitakokanavyo na uzazi kwa asilimia 10.

Pia alihoji serikali imejipangaje kupunguza vifo vitokanavyo na utoaji mimba usio salama?

“Serikali mlisaini Mkataba wa Maputo ‘Maputo Protocol’ kutetea haki za wanawake na uzazi salama, makubalino hayo yalilenga mimba zitolewe zile za kubakwa, shambulio la ngono, mimba maharimu, serikali haioni umuhimu wa kuweka makubaliano hayo katika sheria za nchi yetu ili kuwasaidia wamama wanaopata mimba za namna hii waweze kuzitoa kwa usalama bila kuhatarisha maisha yao? alihoji Conjesta.

Amesema madhara yanayotokana na utoaji wa mimba usio salama ni pamoja na uambukizo mkali wa mfumo wa uzazi (Septic Abortion) ambao unaweza kupelekea mgonjwa kutolewa mfuko wa uzazi maisha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...