Na Mwandishi wetu Dodoma

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma imeanza kambi ya upasuaji wa moyo kwa watu wazima.

Daktari Bingwa wa Moyo wa BMH, Dkt Kelvin Masava, amesema leo kuwa kambi hii ya pamoja ya wiki moja kati ya wataalam wa BMH na wenzao kutoka Uholanzi itahusisha vipimo na matibabu kwa njia ya upasuaji wa kufungua kifua.

"Mpaka sasa, tuna wagonjwa 450 ambao watafanyiwa uchunguzi, watakaokutwa na matatizo watapatiwa matibabu," amesema Daktari huyo Bingwa wa Moyo na kufikia sasa wamewafanyia uchunguzi wagonjwa 146 na wagonjwa wawili wamenufaika na huduma ya upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu kwenye moyo kwa mishipa iliyoziba bila kuusimamisha moyo "Off-pump Coronary Artery Bypass surgery"

Dkt Masava ametoa wito kwa watu wazima wenye matatizo ya moyo katika Kanda ya Kati na mikoa ya jirani waitumie kambi hii ya matibabu katika BMH kwa ajili ya kupata suluhisho.

Dkt Masava ameongeza kuwa lengo la kambi hii ya pamoja na wenzao wa Uholanzi ni kutoa huduma pamoja na kubadilishana uzoefu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...