Timu ya Uhusiano kwa umma kutoka Kampuni ya Blanq Marketing and Communication Agency ikiongonzwa na Mkurugenzi wake, Asinati Eliafie (kushoto) wamekuwa ni miongoni mwa maelfu ya wakimbiaji walioshiriki mbio za Kili Marathon mkoani Kilimanjaro hapo Jana.

Akizungumza baada ya kutimua mbio hizo za nyika, Asinati Eliafie  amesema wamefanya hivyo ili kuwaunga mkono wateja wao ambao pia wamedhamini mbio hizo na wengine wakiwa tu washiriki wa kawaida.

Anaongeza kuwa anafurahi kuona kazi za wateja wao ambazo zinafanywa na Kampuni yao ya Blanq Marketing and Communication zinawafikia maelfu ya Watanzania.

Mbio hizo zenye hadhi ya kimataifa, zimefanyika Jana kwa kuanza na kumalizika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Moshi mkoni Kilimanjaro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...