NA WILLIUM PAUL, MOSHI.

WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi wameonywa kuachana na tabia ya kufanya siasa chafu ya kuwachafua viongozi waliopo madarakani na Chama kitaendelea kuwalinda viongozi hao.

Hayo yamesemwa leo na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI) na Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, Rabia Abdallah Hamid wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro zilizofanyika kata ya Kindi wilaya ya Moshi.

Alisema kuwa, muda wa kufanya kapeni haunafika kwani Chama kinatambua kwa sasa kinawabunge na madiwani na kuwaonya wale wote wenye nia ya kugombea nafasi hizo kusubiri mpaka muda utakapofika.

"Niwaonye wanaccm kuacha tabia ya kufanya siasa chafu kwa viongozi wetu waliopo madarakani sisi tunawatambua waliopo madarakani na tutawalinda ili watimize wajibu wao na kutekeleza Ilani ya CCM" Alisema Rabia.

Na kuongeza "Wabunge na Madiwani hawana shida ila shida wanaletewa na watu wenye uchu wa madaraka ambao wamekuwa wakifanya siasa chafu za kuwachafua sasa niwaonye wanachama wenye nia hiyo kuacha".






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...