Na Mathias Canal, Kiteto-Manyara

Kituo cha afya cha Sunya kilichopo katika Wilaya ya Kiteto kimekabidhiwa magari mawili ya wagonjwa (Ambulance) kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi magari hayo jana tarehe 16 Februari 2024 Mbunge wa jimbo la Kiteto mkoani Manyara Mhe Edward Ole Lekaita amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa magari hayo ili kupunguza adha wanazozipata wananchi.

Amesema Rais Samia ametoa magari matatu ambapo mawili kati ya hayo yamewasili mjini Kiteto, magari mawili yatakuwa kwaajili ya wagonjwa na moja kwaajilia ya madaktari.

Mbunge Ole Lekaita amewataka wahudumu wa afya pamoja na wananchi wote kuhakikisha wanayatunza magari hayo ili yaweze kutumika kuwahudumia kama serikali ilivyokusudia.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe Iddy Kassim pamoja na Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Mhe Priscus Tarimo ambao kwa pamoja wamempongeza Mbunge huyo kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya ya kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

Wamewasihi wananchi kuendelea kumuunga mkono na kumuombea mbunge wao ili aendelee kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...