Mwaka 2024 umeanza kwa rekodi ya ufanisi wa hali ya juu katika kupokea Watalii wanaotumia Bandari ya Kilwa ambapo kwa Mwezi Februari pekee, Meli tano za Watalii zimetia nanga Bandarini hapo na kuhudumiwa.

Bandari ya Kilwa iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, imeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa Watalii kutoka Mataifa mbalimbali ambao wanaendelea kuwasili Nchini kujionea vituo vya Utalii.

Meli ya Watalii ya BOUGAINVILLE ambayo ni Meli ya tano kutia nanga Bandarini hapo, imewasili ikiwa na Watalii 133.

Tangu kuanza kuwasili kwa Meli hizo, jumla ya Watalii 593 Wametembelea Vivutio vya Utalii kwa mafanikio na kusifu huduma za Meli zinazotolewa na Wataalamu Wazawa wa TPA ambao wameonesha Weledi na umahiri mkubwa katika majukumu yao ya kuhudumia Meli hizo za Watalii.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...