Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV



Ameongeza kwamba mradi huo unalenga kuangalia namna bora ya kuyatumia maduka ya dawa kutoa dawa za kujikinga na maambukizi ya Ukimwi ambapo wamelenga watoto wa kike.

"Mradi huu utakuwa ni wa miaka mitano na tutakuwa tunatafuta namna gani bora ya kutumia haya maduka ya dawa kutoa hizi huduma kwa ushirikiano wa haya mashirika niliyoyataja pia kutatengenezwa program itakayowajengea uwezo watalaam katika ngazi ya wilaya na ngazi ya mkoa."
Ameongeza pia kufanya tafiti ambazo zinatokana na wao walivyofanya tafiti mbalimbali ili mwisho wa siku kupata tafiti zitakazosaidia kuboresha sera na miongozo mbalimbali.
"Hivyo tuweze kuwa na miongozo inayotokana na tafiti za ndani ambazo zinaweza kutufanya tuboreshe na kukabiliana na janga la UKIMWI."
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Geita Dk.Omar Sukari amesema katika kikao hicho wamepata nafasi ya kushiriki kwenye kikao cha utambulisho wa mradi ambao unalenga vijana wa kike..
"Kimsingi ni mradi ambao unajielekeza kutanua huduma kuhusu upatikanaji wa dawa za kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa vijana hasa katika mikoa mitatu ambapo mradi unakwenda kutekelezwa.
"Tumefurahi kama waganga wakuu wa mikoa kushiriki kwenye mradi unaokwenda kutekelezwa katika mikoa yetu.
"Ni mradi wa ubunifu ambao unatoa nafasi kwa vijana wa kike ambao wako kwenye rika balehe na wale ambao tayari wameshakuwa vijana wenye umri miaka 28 ili kupata uwezo kuzikifia huduma za kupata dawa za kufubaza maambukizi ya virusi vya UKIMWI, " amesema.
Ameongeza wanajua vijana ni kundi ambalo kwa namna moja au nyingine ndilo hatarishi na asilimia 25 ya maambukizi kwa vijana yako katika kundi hilo.
Hivyo kundi hilo wakilifanyia ubunifu wa kupata dawa hizo kupitia kwenye maduka ya dawa inawezekana kuongeza uwezo wa huduma ambazo watakuwa wanazitoa kupitia maduka hayo.
"Kwa hiyo sisi kama waganga wakuu wa mikoa tunaona ni ubunifu mzuri na utakapokamilika utasaidia Wizara na wadau kutengeneza miongozo ,sera nzuri ya afya namna ya kuwafikia vijana na makundi mengine ambayo yapo kwenye hali hatarishi.
"Kwa hiyo tunadhani ni kitu kizuri, vijana wanakuwa na uhakika wa kupata huduma na itawapa nafasi kwa namna gani waweze kupata huduma."
Kwa upande wake Dk.Eno Machangu amesema mradi huo umelenga kuwafikia vijana na kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma hususani kwa ajili ya vijana rika balehe, vijana wa kike rika balehe kwa lengo la kuwasaidia kupata huduma zaidi za afya lakini kujikinga zaidi na maambukizi ya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...