Na Munir Shemweta, KATAVI

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amewasili mkoani Katavi Katavi leo tarehe 19 Februari 2024 ambapo mbali na mambo mengine atashiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Katika mkutano huo utakaofanyika Februari 24, 2024 katika Shule ya Sekondari Nizengo Pinda-Kibaoni Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM kuanzia Nov 2020 hadi Februari 2023 itawasilishwa na Mhe. Pinda.

Mgeni rasmi katika mkutano huo utakaofanyika anatarajiwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa atazindua Radio ya Halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele itakayojulikana kama Mpimbwe Fm.

Mara baada ya kuwasili mkoani Katavi Mhe, Pinda alikutana na kufanya mazungumzo na mkuu wa mkoa huo Bi. Mwanamvua Mrindoko pamoja na kutembelea ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Katavi.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda (Kulia) akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Katavi Bi. Mwanamvua Mrindoko mara baada ya kuwasili katika ofisi ya mkuu wa mkoa tarehe 19 Februari 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda (Kulia) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa mkoa wa Katavi Bi. Mwanamvua Mrindoko mara baada ya kuwasili ofisi ya mkuu wa mkoa tarehe 19 Februari 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda (Kulia) akisisitiza jambo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Katavi Bi. Mwanamvua Mrindoko mara baada ya kuwasili ofisini kwake tarehe 19 Februari 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akisaini kitabu cha wageni alipowasili ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Katavi tarehe 19 Februari 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akisalimiana na mzee aliyemkuta nje ya ofisi ya CCM mkoa wa Katavi tarehe 19 Februari 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akisalimiana na vijana na umoja wa vijana wa CCM katavi aliowakuta ya ofisi ya CCM mkoa wa Katavi tarehe 19 Februari 2024.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akiwa katika kikao ndani ya ofisi ya CCM mkoa wa Katavi tarehe 19 Februari 2024.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...