






Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Balozi Emmanuel John Nchimbi akiteta jambo na kumsikiliza kwa makini Bi. Fatma Gullam Hussein Jamal (Mama Fatma Karume), ambaye ni Mama Mzazi wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Amani Abeid Karume (kulia), pia Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume, walipokutana msibani kwa Hayati Edward Ngoyai Lowassa, Ngurash, Monduli, Jumamosi, Februari 17, 2024. Dkt. Nchimbi pia alitumia nafasi hiyo kumpongeza Mama Fatma Karume kwa kutimiza miaka 93 ya kuzaliwa hivi karibuni na kumtakia heri, fanaka na maisha marefu zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...