NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amefanya ziara ya kutembelea mradi wenye thamani ya Shilingi 422 milioni wa ujenzi madarasa Saba na matundu 10 ya vyoo katika Shule ya Sekondari ya Mazoezi Chang'ombe iliyopo ndani ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam(DUCE). ambapo ameupongeza uongozi wa Chuo kuhakikisha ujenzi unakwenda kwa kasi na kukamilika kwa wakati.

Akizungumza katika ziara hiyo leo Februari 20, 2024 RC Chalamila amesema uongozi wa shule umejitahidi kusimamia ujenzi wa mradi huo na kuhakikisha fedha ambazo zimetolewa na serikali zinalenga katika ameneo yaliyokusudiwa.

Amesema kuwa Serikali imekuwa ikijitahidi kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu iliyobora ndo maana wamekuwa wakijitahidi kuboresha madarasa na vyoo katika shule mbalimbali nchini ili kumuondolea changamoto mwanafunzi.

"Wengine wanaishi mbali na shule wanazoenda kusoma, tumekuja na mpango wa kujenga hosteli kila shule, kwanza kujenga nidhamu ya taaluma kwa wanafunzi". Amesema
 
Aidha amesema wameanzisha mpango wa kujenga hosteli za wanafunzi kwa shule zote ili kujenga nidhamu ya taaluma na kutengeneza mazingira mazuri ya kujadili kuhusu kesho yao.

Ambapo amesema mpango huo utaenda sambamba na kujenga shule maalum kwa ajili ya Wanafunzi wanaopata sifuri kwenye mitihani yao ya mwisho itakayosajiliwa kwa mfumo wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Awali, akisoma taarifa za shule hiyo Rasi wa Chuo cha DUCE, Profesa Stephen Maluka amesema madarasa hayo saba yatasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika madarasa.

"Tuna wanafunzi wengi zaidi ya 1000 na idadi imekuwa ikiongezeka kutokana na uhitaji na haya madarasa Saba yataweza kuchukua wanafunzi 180 na ujenzi wake ulianza mwaka 2019 umekuwa ukienda taratibu kwakuwa tunategemea fedha kutoka mapato ya ndani na Serikali," amesema
 












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...