Na. Beatus Maganja 

Kwa miongo kadhaa kumekuwa na dhana ya kwamba wageni wengi wa nje hupendelea zaidi utalii wa kuona wanyamapori, lakini hivi karibuni dhana hiyo imeanza kubadilika kwa kasi ambapo Tanzania imeanza kupokea wageni makundi kwa makundi wakitembelea katika maeneo yetu ya Malikale hususan Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara.

Ni takrikani siku 9 sasa katika kipindi cha Mwezi Februari kuanzia tarehe 03 - 11, 2024, Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imeweza kushuhudia   Meli zilizosheheni makundi ya Watalii kutoka Mataifa mbalimbali zikipishana kutia nanga katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara na kufikisha idadi ya watalii wapatao 445 kwa safari nne (4) za kitalii zilizofanyika.

Kwa mara nyingine Februari 11, 2024 TAWA ilipokea kundi la nne (4) la watalii wapatao 114  kutoka Ufaransa ambao waliingia Kilwa kisiwani kwa ajili ya shughuli za utalii na kufanya idadi ya watalii wa nje waliotembelea hifadhi hiyo ndani ya siku 9 tu kuwa 445.

Hata hivyo, TAWA inategemea kuendelea kupata wageni wengi kutoka Kona mbalimbali za Dunia kuja kutembelea na Kutalii Katika Hifadhi hiyo kongwe yenye utajiri mkubwa wa kihistoria.

Kwanini Kilwa Kisiwani na Songo Mnara? Wahenga walisema ukitaka kuujua uhondo wa ngoma, uingie ucheze, hivyo TAWA inaendelea kuwakaribisha watalii wote wa ndani na nje kutembelea hifadhi hii kujionea  yaliyomo.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...