Zanzibar, 23 Machi 2024. Benki ya Equity katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani imefuturisha wateja wake katika mji mkongwe wa Zanzibar ikiwa ni ishara ya shukurani kwa wateja na wadau wake wa karibu kwa kuendelea kuichagua benki hiyo kama benki yao pendwa.

Akiongea kwenye hafla hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw. Rojas Mdoe amesema kwamba Benki ya Equity Tanzania inathamini mchango wa wateja wakekatika ukuwaji wa amana za benki na kwa kutumia huduma za benki. Akaendelea kusema, dhumuni kubwa la kuandaa Futari hii ni kuwashukuru wateja wake kwa kuwa bega kwa bega kuhakikisha tunabadilisha maisha ya kila Mtanzania.

Aliendelea na kusema kuwa benki yetu inaendelea kuboresha huduma zake na kuhakikisha kuwa inatanua wigo wake wa upatikanaji nchini ili kuweza kuwafikia wateja wote Tanzania na kuhakikisha kuwa inatimiza dhamira yake ya kubadilisha maisha ya kila Mtanzania.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Afisi ya Raisi Kazi, Uchumi na Uwekezaji Mh. Sharif A. Sharif alisema, nawapongeza sana benki ya Equity kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kukuza uchumi wa taifa letu kwa kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anatumia mifumo rasmi ya kifedha (financial inclusion). Vilevile kwa ubunifumkubwa wa kutoa huduma bora za kibenki za kidijitali.

Kuhusu Benki ya Equity

Equity Bank (T) ni Benki yenye matawi 16 nchini, mawakala zaidi ya 2,000 ikiwa na zaidi ya wafanyakazi zaidi ya 400 ikiwa ni moja ya uwekezaji mkubwa zaidi ulioanzia nchini Kenya na baadaye kusambaa katika nchi nyingine 5 za Afrika Mashariki, ikiwemo Tanzania, Uganda, Congo-DRC, Rwanda na Sudan ya Kusini.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...