Na. Damian Kunambi, Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Victoria Mwanziva akiambatana na Mkurugenzi wa Halamashauri, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi wilayani humo wamefanya Dua/Kisomo Maalum cha kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ili azidi kupata kheri, hekmana baraka.

Akizungumza mara baada ya kufanyika kisomo hicho katika msikiti wa Wilaya ya Ludewa mkuu huyo wa wilaya amesema Rais Dkt. Samia amekuwa ni kiongozi anaye liongoza vyema Taifa la Tanzania hivyo anapopata baraka taifa zima linapata baraka pia kupitia yeye.

"Rais wetu amekuwa ni kiongozi bora na mwenye hekma, hivyo hatuna budi kumwombea kwa Mungu ili aweze kuendeleza ubora alio nao na kile ambacho Mungu amekiweka ndani yake".

Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya hiyo Sunday Deogratius amempongeza mkuu huyo wa Wilaya kwa kuandaa kisomo hicho kilicho ambatana na futari na kuongeza kuwa Rais Dkt. Samia amefanya maendeleo makubwa katika halmashauri mbalimbali ikiwemo halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ambayo imepiga hatua kwenye maendeleo ya elimu, afya, miundombinu ya barabara na sekta nyinginezo.

Aidha kwa upande wake shekhe wa Wilaya hiyo Haruna Rahim amemshukuru mkuu wa wilaya kwa kuwaunganisha katika kufanya kisomo hicho pamoja na kupata futari kwani kwa kufanya hivyo kunaongeza Swawabu kutoka kwa mwenyezi Mungu na hasa katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhan.

Kisomo hicho cha kumwombea Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kiliambatana na Iftari iliyo andaliwa na mkuu huyo wa Wilaya Victoria Mwanziva katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo waumini wote wa kiislamu na wageni waalikwa walijuika pamoja kupata ftari hiyo.

Sanjari na kisomo hicho na futari lakini pia mkuu huyo wa Wilaya alimkabidhi Shekhe Haruna zawadi ya pikipiki aina ya King lion 150 yenye thamani ya shilingi 2,600,000 milion ili iweze kumsaidia katika mizunguko yake mbalimbali huku mbunge wa jimbo la Ludewa akitoa hundi ya shilingi 1,000,000 kwaajili ya ujenzi wa msikiti.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...