Angela Msimbira GEITA

KAMATI ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (LAAC) imetoa miezi 3 kwa Halmashauri ya Mji wa Geita kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Bulela kilichopo katika Kata ya Bulela mkoani Geita.

Agizo hilo limetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Staslaus Mabula wakati wa majumuisho ya ziara ya Kamati ya LAAC ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Mji wa Geita, mkoani Geita.

Amesema kuwa kituo hicho kitaendelea kutoa huduma huku kikiendelea kufanyiwa marekebisho mbalimbali ikiwemo kubadilisha sakafu na milango ambayo haina ubora.

Mabula pia ameishauri Halmashauri hiyo kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaa tiba ili kituo hicho kinapokamilika kiweze kuwa na vifaa vitakavyoweza kutoa huduma bora kwa jamii

Pia imependekeza chumba cha upasuaji kikamilishwe kwa wakati na kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa vifaa ili kuanza kutoa huduma za upasuaji kwa mama wajawazito.

"Chumba cha upasuaji ni eneo muhimu sana kwa kuwa huko ndipo tunapowalenga wamama wajawazito wenye changamoto kupata matibabu hivyo hakikisheni inakamilika na vifaa vinakuwepo," amesisitiza Mabula.

Aidha, Mabula amewataka kuhakikisha wanajibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na za kamati ili kuzifuta na kuziondoa kabisa.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...