Na Munir Shemweta, NZEGA


 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) katika halmashauri ya Mji wa Nzega mkoa wa Tabora.

 

Kauli hiyo imetolewa tarehe 27 Machi 2027 wilayani Nzega na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe, Japhet Hasunga wakati wa ziara ya Kamati yake kukagua hatua iliyofikiwa katika Utekelezaji mradi wa LTIP kwenye halmashauri ya Mji wa Nzega mkoani Tabora.

 

Mradi wa LTIP katika Halmashauri ya Mji wa Nzega umepewa lengo la kurasimisha vipande vya ardhi 20,000 na kuongeza alama za msingi za upimaji 14.

 

"Niwapongeze kwa kazi hii mlioamua kuifanya tangu tupate uhuru tumekuwa na changamoto za ardhi kuanzia kutambua, kupima, kurasimisha na kadhalika, kumekuwa na shida" amesema Mhe, Hasunga.

 

Amesema, Mhe, Rais ameamua kutoa fedha nyingi za mradi wa LTIP na Bunge kuidhinisha ambapo kwa upande wa halmashauri ya Mji Nzega kiasi cha Shilingi Bilioni 1.4 kimeidhinishwa kwa ajili ya Kata tano hivyo wananchi watumie fursa ya kutambuliwa maeneo yao na hatimaye kupatiwa hati kupitia mradi huo.

 

Ameeleza kuwa, Kamati yake ya PAC itakwenda kupima thamani ya fedha zilizopitishwa na Bunge pale tu wananchi watakapokuwa na hati.

 

"Msipopata hati hii mingine yote ni michakato, sisi hatuhitaji michakato tunataka kuona watu wangapi wana hati" alisema Mhe, Hasunga.

 

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda amesema, wizara yake ina uhakika michakato yote itakapokamilika katika mji wa Nzega hati milki za ardhi zitaenda kutolewa kwa wananchi.

 

Kwa mujibu wa Mhe, Pinda utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) unaenda kutoa jumla ya hati milki za ardhi 1,500,000 kwa maeneo yote yanayopotiwa na mradi.

 

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga ameweka wazi kuwa, kazi iliyofanyika kwa halmashauri ya Mji wa Nzega kwa sasa imefikia asilimia 55 na kiasi cha fedha kilichotolewa ni asilimia 39.

 

Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) unatekelezwa kwa mkopo wenye thamani ya Dola za Kimarekani milionin150 kutoka Benki ya Dunia kwa kupindi cha miaka 5 katika halmashauri 58 nchini. Mradi huo unalenga kuboresha utawala na usimamizi wa ardhi nchini pamoja na kuongeza usalama wa milki za ardhi kwa wananchi.Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe, Japhet Hasunga akisalimiana na waratibu wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) alipowasili na Kamati yake kukagua hatua iliyofikiwa katika Utekelezaji wa Mradi huo  Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024.Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe, Japhet Hasunga akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Mhandisi Anthony Sanga na Naibu Waziri Mhe, Geophrey Pinda wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali ilipokwenda kukagua hatua iliyofikiwa katika Utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024.Sehemu ya washiriki wa ziara Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali ilipokwenda kukagua hatua iliyofikiwa katika Utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024.

Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali ilipokwenda kukagua hatua iliyofikiwa katika Utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...