Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Wananchi, Viongozi mbalimbali wa Kitaifa akiwemo Makamu wa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, Makamu Mwenyekiti CCM (Bara) Ndugu Abdulrahman Kinana, Mama Mariam Mwinyi na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam kuaga Mwili wa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi.

Shughuli hiyo ya kuaga mwili imehudhuriwa pia na Mabalozi wanaowakisha nchi zao Tanzania, Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Viongozi wa Dini.

Mzee Mwinyi amefariki dunia jana tarehe: 29 Februari 2024 katika hospitali ya Mzena, Kijitonyama, Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

 








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...