Afisa Uhusiano na Mawasiliano - TCAA Maureen Peter Swai(kushoto) akikabidhi msaada kwa Mkurugenzi wa Kituo cha kulelea watoto cha Zili House Emanuel Zadock (kulia) ikiwa ni kurudisha kwenye jamii kwakusambaza upendo na tabasamu kwa watoto yatima wa kituo hicho kilichopo eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam. Msaada uliotolewa na TCAA ni mchele, Unga, mafuta ya kula, Taulo za Kike, sabuni, ngano nk.
Afisa Uhusiano na Mawasiliano - TCAA Maureen Peter Swai akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada katika kituo cha kulelea watoto cha Zili ikiwa ni kurudisha kwenye jamii kwakusambaza upendo na tabasamu kwa watoto yatima wa kituo hicho hasa kwa kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka na Idd 
Mkurugenzi wa Kituo cha kulelea watoto cha Zili House Emanuel Zadock akizungumzia historia pamoja na kutoa shukrani kwa viongozi pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwa kuweza kutoa msaada kwenye kituo hicho kilichopo eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.

Dorethea ponela Daniel akitoa neno la shukrani wa viongozi pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwa kuweza kuwapatia msaada kituo hicho kilichopo eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) pamoja na watoto  wakisikiliza historia ya Kituo cha kulelea watoto cha Zili House wakati wa hafla ya kutoa msaada  katika kituo hicho
 Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)  wakiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa Kituo cha Zili House pamoja na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho mara baada ya kukabidhi msaada ikiwa ni kurudisha kwenye jamii kwakusambaza upendo na tabasamu kwa watoto yatima wa kituo katika kituo hichokilichopo eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...