Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, akisikiliza na kujibu maswali ya wananchi mbalimbali waliojitokeza barabarani kumsalimia wakati akiwa njiani, eneo la Mlowo, Mbozi, wakati akitokea Vwawa, Mbozi, kuelekea Mbalizi, mkoani Mbeya tayari kuanza ziara ya siku 2 mkoani humo, leo Jumanne, Aprili 16, 2024, baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili pia, mkoani Songwe. Dk. Nchimbi, ambaye ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Oganaizesheni, Issa Haji Usi Gavu na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Gabriel Makala, yuko katika ziara ya mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...