Na Shalua Mpanda

MKUU wa Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam Sixtus Mapunda ameonesha kukasirishwa na tabia ya madereva wa malori na wamiliki wa viwanda kuegesha malori pembezoni mwa hifadhi ya barabara.

Akiwa katika ziara ya kushtukiza katika eneo la barabara ya Mbozi iliyopo kata ya Chang'ombe wilayani humu leo Aprili 16,2024 , Mapunda amesema, umefika wakati wa kila mmoja kuheshimu Sheria zilizowekwa ili kuepusha kero kwa watumiaji wengine wa barabara.

"Nimeshatoa maagizo,hawa wote walioegesha magari yao pembezoni mwa hii barabara,Mamlaka husika zichukue hatua stahiki....leo hii hapa ikitokea ajali ya moto gari za zimamoto zitaweza kupita hapa?"Alihoji Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha Mapunda amewataka wenye viwanda na bandari kavu kuweka utaratibu wa kuwa na maeneo maalumu kwa ajili ya maegesho ya malori wakati wa kusubiria kuingia kwenye viwanda hivyo.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi walioongea na mwandishi wa habari hizi walisema uegeshaji huo
umechangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa miundombinu ya barabara hiyo.

Barabara hiyo muhimu ya Mbozi imekuwa na msongamano mkubwa wa malori hasa nyakati za asubuhi na jioni kutokana na malori mengi yakiwemo mabovu kuegeshwa pembezoni hali inayochangia kwa kiasi kikubwa foleni hiyo.



 

Mkuu wa Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam Sixtus Mapunda akiwa katika ziara ya kikazi,akikaangalia uegeshaji malori ambao ameoneshwa kukerwa nao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...