NA WILLIUM PAUL, SAME.

MKUU wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni ameliagiza Jeshi la polisi kufanya msako na kuwakamata watu watatu wa familia moja wanaotuhumiwa na kwa maua ya Mwenyekiti wa kitongoji cha Kampimbi kata ya Ndungu, Charles Johnson Mkuruto(58).

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa wilaya, mnamo Aprili 26 mwaka huu majira ya saa tano na nusu asubuhi huko kitongoji cha Kampimbi kijiji cha Ndungu kata ya Ndungu mtu mmoja aitwae Johnson Mkuruto(58) Mwenyekiti wa Kitongoji cha Sinangoa 'A' aliuwawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya kichwani na nyuma ya bega la kulia.

Alisema kuwa, Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Ardhi kata ya Ndungu alikatwa na watu watatu ambao aliwataja kwa majina kuwa ni Mohamad Makundi, Hamad Makundi na Mnandi Makundi na kutoweka kusikojulikana.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa, sababu ya mauaji hayo ni mgogoro wa Ardhi uliopo Mahakama ya Ardhi ya Ndungu.

"Baraza la Ardhi jana lilienda eneo la mashamba yanayobishaniwa ndipo watuhumiwa walimvamia marehemu na kumkatakata na kitu chenye ncha kali kisha kukimbia" Alisema Kasilda. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...