Na Mwandishi Wetu, Arusha

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), imetoa mafunzo maalumu kwa akina mama lishe 50 wa mkoa wa Arusha kwa lengo la kuwaelimisha namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali ya moto.

Mbali na mafunzo hayo, pia GGML imewagawia mitungi 50 ya gesi ya kupikia kwa ajili ya kuhamasisha akina mama hao kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kisha kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi.

Mafunzo hayo yalitolewa jana katika maadhimisho ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yanayofanyika Kitaifa Jijini Arusha kuanzia tarehe Aprili 23 hadi Mei Mosi 2024.

Akizungumza na akina mama lishe hao, Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi amesema wamemua kutoa elimu kwa akina mama hao ili watambue namna ya kupambana na moto majumbani na kuzingatia usalama kwenye maeneo yao ya biashara hasa ikizingatiwa wao ni chanzo kikubwa cha kukutana na watu wengi.

“Tunawafundisha namna ya kupambana na majanga ya moto kwani shughuli zao za kila siku zinahusiana na masuala ya moto na matumizi ya mkaa na gesi.

“Lakini pia ni vema kutambua namna gani mabadiliko ya tabia nchi yanaathiri watu pia namna tabia zetu binafsi zinavyoweza kuchangia kuachana na ukataji hovyo wa miti,” amesema.

Amesema athari za mabadiliko ya tabia nchi, zinamuathiri kila mmoja bila kujali, cheo, mkubwa au mdogo hivyo ni vema kila mmoja kuzingatia matumizi ya nishati safi ili kuondokana na majanga yatokanayo na mabadiliko hayo.

“Tumeandaa elimu hii kuona namna ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa sababu ukataji wa miti ukikithiri unasababisha mmonyoko wa ardhi, mafuriko na ongezeko la joto duniani.

“Matumizi ya mkaa au kuharibu vyanzo mbalimbali ambavyo vinaweza kusabababisha athari kwenye mazingira na kusababisha mafuriko hata kwenye maeneo yetu ya uchimbaji,” amesema.

Kwa upande wa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi amesema katika mafunzo hayo, wamewafundisha akina mama hao namna salama ya kutumia nishati ya gesi na kuwasisitiza kuondokana na matumizi ya mkaa.

“Lakini pia kwenye banda letu tumeendelea kupokea wageni wanaopenda kujifunza namna ya kupambana na majanga ya moto kwa sababu asilimia kubwa wanauelewa mdogo namna ya kukabiliana na majanga ya moto majumbani,” amesema na kuongeza;

“Watu wengi hawajui njia za awali za kupata msaada wa kuzima moto, sisi tunatoa mafunzo hayo, kuna vifaa vya kawaida ambavyo mama yeyote anavyo nyumbani, mfano ndoo ya maji, taulo, kanga au kitenge vilivyolowekwa kwenye maji, ni vifaa vya kawaida ambavyo unaweza kutumia kuzima moto hivyo tunaendelea kuwaribisha kwenye mabanda yetu,” alisema.

Wakati huo huo Mkaguzi wa afya ya mazingira ya kazi kutoka OSHA, Elizabeth Mtile amewasisitiza akina mama hao kuzingatia umuhimu wa kufuata sheria na miongozo mbalimbali ya usalama na afya katika maeneo ya kazi.

“Kauli mbiu yetu inayosema athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama na afya kazini, inalenga kudhibiti majanga na mabadiliko haya ya tabia nchi kwa kushirikisha kila kundi kwenye jamii kwani athari hizi zinatugusa sisi sote,” amesema.

Mmoja wa akina mama lishe hao, Prinsila Kwai aliishukuru GGML na OSHA kwa kupatia mafunzo hayo kwani yanaenda kuwa chachu ya mabadiliko kwao na kwa wale wanaowazunguka.

“Kwa kweli tunashukuru sana kwa shughuli zetu za kila siku zinahusiana na moto hivyo mafunzo haya yatatusaidia sana namna ya kukabiliana na mlipuko labda wa gesi,” amesema.
 

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.
 

Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi akimgawia mtungi wa gesi ya kupikia mmoja wa akina mama lishe waliopatiwa mafunzo ya namna ya kuzima majanga ya moto wakati wanapoendelea na shughuli zao za kupika. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha ambao pia wote waligawiwa mitungi ya gesi.
 

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akiwaonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.
 

Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk. Kiva Mvungi (kulia) akizungumza na akina  mama lishe kuwaeleza namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...