Serikali imezipongeza Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Kamati za Maafa katika maeneo yote yaliyokumbwa na maafa ya mafuriko kwa namna wanavyosimamia zoezi la uokoaji na kuratibu kwa makini misaada inayotolewa kwa ajili ya waathirika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo ametoa pongezi hizo wilayani Rufiji, wakati aliposhuhudia Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge akipokea msaada wa tani 20 za chakula na Mitungi ya Gesi na Majiko yake 300 iliyotolewa na Kampuni ya Lake Energies kwa ajili ya wananchi wa wilaya ya Rufiji waliokumbwa na mafuriko.
Dkt. Jafo amesema misaada hiyo ni kielelezo cha wadau na wawekezaji nchini kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye yeye mwenyewe Rais amekuwa kiongozi katika kuchangia misaada hiyo kwa ajili ya watanzania wa maeneo mbalimbali yaliyokumbwa na changamoto ya mafuriko kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Serikali imezipongeza Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Kamati za Maafa katika maeneo yote yaliyokumbwa na maafa ya mafuriko kwa namna wanavyosimamia zoezi la uokoaji na kuratibu kwa makini misaada inayotolewa kwa ajili ya waathirika.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo ametoa pongezi hizo wilayani Rufiji, wakati aliposhuhudia Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge akipokea msaada wa tani 20 za chakula na Mitungi ya Gesi na Majiko yake 300 iliyotolewa na Kampuni ya Lake Energies kwa ajili ya wananchi wa wilaya ya Rufiji waliokumbwa na mafuriko.

Dkt. Jafo amesema misaada hiyo ni kielelezo cha wadau na wawekezaji nchini kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye yeye mwenyewe Rais amekuwa kiongozi katika kuchangia misaada hiyo kwa ajili ya watanzania wa maeneo mbalimbali yaliyokumbwa na changamoto ya mafuriko kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...