JITIHADA za Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe Miraji Mtaturu kwa kushirikiana na wanachi zimesaidia kukamilisha kazi ya upauaji wa madarasa mawili katika Shule Shikizi ya Mwitumi hatua itakayoondoa changamoto ya watoto kusafiri umbali wa kilomita 9 na kuvuka mito miwili kufuata shule mama ya Msingi Nkundi.

Katika jitihada hizo wananchi walitumia nguvu yao kujenga hadi usawa wa Lenta na mbunge akawaunga mkono kwa kutoa Sh Milioni 13 ambazo zilinunua Bati 110, mbao zote na Saruji ya kupiga lipu na Sakafu.

Akizungumza na kituo hiki April 24,2024,Mtaturu amesema kukosekana kwa madarasa hayo kumesababisha utoro wa wanafunzi wakati wa masika na hivyo kushusha kiwango cha ufaulu.

Amewashukuru wananchi wa Kitongoji cha Mwitumi, Kijiji cha Nkundi Kata ya Kikio kwa Ushirikiano mkubwa walioutoa wa kushirikiana nae na kumaliza shughuli ya ujenzi wa Darasa

"Hatimaye imewezekana kwa kushirikiana na wananchi tumepaua vyumba viwili vya madarasa katika kuhakikisha changamoto ya watoto wanaosafiri mwendo mrefu na kuvuka mito miwili kufuata shule mama ya Msingi Nkundi inaisha,nawashukuru sana wananchi kwa jitihada zenu,".ameshukuru.

#VitendoVinasautiKulikoManeno#SingidaMashariki#TunaendeleaKuwafikia#

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...