Na Mwandishi Wetu 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi (NEEC) Bi Beng'i Issa amesema kuwa katika miaka sita ya Rais Dkt.SamiaSuluhu Hassan kimekuwa na mapinduzi katika uwekeaji nchini kwa wazawa.

Beng'i ameyasema hayo wakati wa akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu kongamano la nne la Ushiriki wa Watanzania kwenye uchumi na Uwekezaji (Local Content) litakalofanyika kuanzia tarehe 27 hadi 28 mwezi huu

Amesema kuwa Kongamano hilo hufanyika kila baada ya miaka miwili ikiwa ni pamoja kuangalia tathimini ya miaka miwili iliyopita na kuweka dira ya miaka miwili katika uwekezaji kwa wazawa.

Amesema , mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati , Dkt Dotto Mashaka Biteko.

Amesema kuwa Kongamano hilo litaweka picha ya kuweza kukua Kwa uwekezaji wa wazawa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi (NEEC) Bi. Beng'i Issa akizungumza na waandishi wa habari ( hawapo picha) kuhusu kongamano la nne la Ushiriki wa Watanzania kwenye uchumi na Uwekezaji (Local Content) litakalofanyika kuanzia tarehe 27 hadi 28 mwezi huu ambalo hufanyika  Kila baada ya miaka miwili , mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati , Dkt Dotto Mashaka Biteko .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...