NAIBU Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Dkt Festo Dugange amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa itatenga Sh Milioni 100 kwa ajili ya kuongeza majengo na kuanza utaratibu wa kupandisha hadhi zahanati ya Madope kuwa kituo cha afya.

Mhe Dkt Dugange ametoa kauli hiyo leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Ludewa, Mhe Joseph Kamonga aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kupandisha hadhi Zahanati za Madope na Ludewa kuwa vituo vya afya.

“ Zahanati za Madope na Ludende ni Zahanati zilizopo kwenye Makao Makuu ya Kata za Madope na Ludende Mtawalia. Zahanati ya Madope ina eneo la takribani ekari 10 pamoja na vigezo vingine inakidhi kuwa na kituo cha afya.

Katika mwaka wa fedha 2025/26 serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo itatenga Sh Milioni 100 kwa ajili ya kuongeza majengo na kuanza utaratibu wa kuipandisha hadhi kuwa kitio cha afya,” Amesema Mhe Dkt Dugange.

Kuhusu Zahanati ya Ludende amesema haikidhi vigezo vya kuwa kituo cha afya kwa kuwa ina eneo dogo (ekari 5), uchache wa watu na inapakana na kituo cha afya Mlangali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...