Na Mwandishi Wetu

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu Gungu Silanga amewataka madiwani na wabunge walioko Wilaya ya Bunda mkoani Mara kutokuwa na mashaka na watu wanaopita kupiga kelele na badala yake wafanye kazi kwani wananchi wanaona utekelezaji wa Ilani unaendelea kufanywa na Serikali ya Chama hicho.

Silanga ameyasema hayo leo Aprili 15,2025 katika kikao cha ndani ya Wanachama wa CCM Wilaya ya Bunda mkoani Mara baada ya kupewa nafasi ya kusalimia wanaCCM hao waliohudhuria kikao kazi cha Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Abdulrahman Kinana ambaye yuko katika ziara katika wilaya hiyo akitokea Serengeti. Rorya, Tarime na Butiama.

“Wana Bunda kwanza nawapongeza kwa ushindi ambao umeupata mwaka 2020 kwa kupata madiwani na wabunge wengi.Watu wa Bunda wako timamu na sidhani kama kutakuwa na shida yoyote, wana Bunda ni wachapakazi , wapambanaji na mfumo wa Chama chetu ni kufanya kazi kwa uwazi na ukweli.

“Madiwani na viongozi wengine fanyeni kazi ya kutekeleza llani ya 20220, wanaopita na kupiga kelele achaneni nao, ukifanya kazi wananchi na wana CCM wanaona.Fanyeni kazi Chama kipo imara, Rais Samia Suluhu Hassan yuko imara na Kamati ya siasa Wilaya ya Bunda inafanya kazi,”amesema.

Pia amewahimiza wanaCCM kuendelea kushikamana kwani Chama hicho ili kiendelee kushika dola ni pale tu ambapo kuna muungano.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...