Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi  ameipongeza Jumuiya  ya  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kazi kubwa waliyoifanya kuwaletea maendeleo wanawake na kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuandaa mdahalo wa wanawake na Muungano.

 Pia, ameupongeza umoja huo kwa kuendelea kuwa kinara katika kubuni na kutengeneza mambo mbalimbali yenye lengo la kuimarisha CCM, kikiunganisha na wananchi na kuimarisha umoja na mshikamano na wananchi.

Dkt. Mwinyi amesema hayo jijini Dar es Salaam leo Aprili 25, 2024 alipofungua mdahalo wa kitaifa wa Wanawake na Muungano uliondaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City.

Mdahalo huo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wake za viongozi  wakuu wastaafu, mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wawakilishi, wananchi na wanachama wa jumuiya hiyo na wa CCM.

Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda amesema wanafanya mdahalo wa kuelekea miaka 60 ya Muungano na kujadili nafasi ya mwanamke katika kipindi cha nyuma,sasa na kijacho

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa UWT, Ndg.Zainab Shomari amesema muungano huo uliletwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar zikiwa huru, haukuwa wa kuchanganya mchanga tu, bali wa kidamu  kwa kuwa Zanzibar kuna watu wa makabila mbalimbali.

 

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwasilimia Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  walipowasili katika ukumbi wa mkutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kulifungua Kongamano la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo.(Picha na Ikulu)
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akiwa na Wake wa Viongozi wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifungua Kongamano hilo lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Kongamano na Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishingilia wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan, akipokewa kwa niaba Mhe.Wanu Hafidh Ameir, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi,akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume Mama Fatma Karume,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)  
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhiwa Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa mchango wake, akikabidhiwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatanda, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano  kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,i lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
VIONGOZI Wastaafu wa UWT wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024 na kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, lililofanyika katika ukumbi wa Mlomani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...