Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU), Dkt. Paul Loisulie,akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Uchambuzi na Mapendekezo ya hoja za NHIF na Pensheni nchini Tanzania.
Na Mwandishi Wetu

KUELEKEA Bima ya Afya kwa Wote Chama Cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu (THTU) imeshauri serikali kuendelea kuchukua hatua kali dhidi ya watu wanaotumia vibaya fedha za mifuko ya bima ya afya ili kukomesha tabia hiyo.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa THTU Taifa Dk. Paul Loisulie, wakati akitoa Mapendekezo ya Hoja Za NHIF na Pensheni Nchini Tanzania.

Alisema pamoja na changamoto zote na dalili isiyo nzuri juu ya Bima ya Afya kwa wote, THTU inaamini kuna mambo ya kufanyika kwa utashi sahihi na nia thabiti ili kuwezesha Bima ya Afya kwa wote ifanye kazi kwa ufanisi mkubwa.

“Serikali iwe na hasira na wivu juu ya rasilimali zinazotapanywa kila mara katika mifuko hii na kuchukua hatua ya kukomesha.

Aliongeza kuwa :”Isisubiri ripoti ya CAG bali ichukue hatua mapema. Serikali pia iepuke utaratibu wake wa kukopa au kujichotea pesa kutoka kwenye mfuko ili pesa hizo zitumike kugharamia huduma za afya tun a si vinginevyo,”

Loisulie alishauri Bunge litimize wajibu wake kikamilifu katika kutunga sheria rafiki kwa wafanyakazi na wanajamii Pamoja na kuisimamia serikali katika usimamizi wa mifuko husika.

Alisisitiza kuwa Bunge halipaswi kuwa sehemu ya kulalamika bali kutatua changamoto zinazojitokeza

Katika hatua nyingine alisema upo ulazima wa Wafanyakazi, wanajamii na wanufaika wote wa Bima kuamka usingizini na kuacha tabia ya kugugumia chini kwa chini huku Mfuko ukiteketea.

“Ijengeke tabia ya kuhoji na kushinikiza uwajibikaji pale matumizi mabaya na usimamizi usioridhisha inapobainika na mamlaka zinazoaminika kama CAG,”alifafanua .

Aliongeza kuwa :” Ifanyike mijadala ya wazi na shirikishi kuhusu uhai wa mfuko mara kwa mara ili kubaini changamoto na namna ya kuzitatua badala ya kuachia mfuko peke yake. Hii itahusisha pia kutumia ripoti za kitaalamu za tathmini juu ya mwenendo wa mfuko,”.

Kuhusu Kikokotoo, (THTU) imependekeza Kikokotoo kifanyiwe mabadilko kwa kuongeza umri baada ya kustaafu toka miaka 12.5 hadi 15.5 na wanachama wapewe angalau 50% kama mafao ya mkupuo.

amesema "Kuhusu hoja ya Kikokotoo kinachotumika hakiakisi hali halisi ya wanachama – kanuni 8(1)(a)(b)(c) (a) kigezo cha umri (b) kigezo cha malipo ya mkupuo mapendekezo yao ni Kikokotoo kifanyiwe mabadilko kwa kuongeza umri baada ya kustaafu toka miaka 12.5 hadi 15.5."amesema Dkt.Loisulie
Pia wanachama wapewe angalau 50% kama mafao ya mkupuo itumike 1/540 badala ya 1/580.
Kuhusu Waziri husika kuwa na mamlaka ya kuamua kiwango cha michango ya mwanachama katika mfuko wanapendekeza Kifungu kidogo cha 18(2)(b) kiondolewe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...