Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alizindua Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na mifumo ya usajili na malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi katika kituo cha Mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 03 April 2024

Tukio hili lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mawaziri, mabalozi, pamoja na wageni mbalimbali.

Makampuni, mashirika, na taasisi mbalimbali zimetunukiwa cheti cha usajili kwenye Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Moja ya makampuni yaliyotunukiwa Cheti hicho ni Vodacom Tanzania. Hii ni baada ya kuwa kampuni ya mwanzo kusajili ulinzi wa taarifa binafsi za wateja wake hapa Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan akimkabidhi cheti cha usajili wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mkurugenzi wa kitengo cha Sheria wa Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC Olaf Mumburi mara baada ya kuzindua tume hiyo jijini Dar es Salaam tarehe 3 April mwaka huu.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Vodacom wakiwa katika eneo la hafla mara baada ya kukabidhiwa cheti cha usajili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...