Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Serikali ilianza rasmi kuratibu utekelezaji wa Programu ya Taifa ya Mafunzo ya Uzoefu wa Kazi kwa wahitimu (internship) mwaka 2019/2020.

Aidha, tangu kuanza kwa utekelezaji wa programu hiyo jumla ya Wahitimu 21,280 wamenufaika ambapo wanaume ni 11,281, wanawake 9,999 na Miongoni mwa wanufaika hao jumla ya Wahitimu 3,772 wamepata kazi Serikalini, Sekta Binafsi na nje ya Nchi.
Mhe. Ndejembi amebainisha hayo leo Aprili 18, 2024 Bungeni Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Shally Joseph Raymond lililohoji, Wahitimu wangapi wa Vyuo wanafanya kazi ya kujitolea na wangapi wameajiriwa na kujiajiri baada ya kujitolea.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...