Askofu Mkuu wa Kanisa la Calvary Assemblies of God, Mtume Dkt. Dunstan Maboya akiambatana na Viongozi wengine wa kanisa hilo wameongoza maombi Maalum ya kumuombea Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda na kuwatakia mafanikio mema kwenye kuwatumikia wananchi.

Askofu Dkt. Dunstan Maboya amefika Ofisini kwa Mhe. Paul Makonda, mkuu wa Mkoa wa Arusha akiambatana na Mchungaji Daniel Safari na Nabii Joshua Alamu ambaye ni Rais wa Baraza la Mitume na Manabii nchini Tanzania.

Viongozi hao wa dini Wakiongozwa na Askofu Maboya wameiombea pia mihimili yote ya nchi kwa maana ya Bunge, Mahakama na Serikali na kuwataka kutenda Haki katika kuwatumikia Watanzania.

Aidha Baba Askofu Dunstan Maboya ametumia fursa hiyo kumualika Mhe. Mkuu wa Mkoa kwenye Tamasha kubwa la Muziki wa Injili linalotarajiwa kufanyika Juni 2 mwaka huu Jijini Arusha likitanguliwa na Kongamano la dini linalotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Paulo Christian Makonda akisalimiana na Mkuu wa Makanisa ya Calvary assemblies of God alipotembelea katika Ofisi hiyo mapema Leo.
Katika picha ni Mtume Dastan Maboya Askofu Mkuu wa Makanila ya Calvary Assemblies of God akiwa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda wakiwemo viongozi wa dining wengine ambao wametmbelea katika ofisi ya Mkuu huyo wa mkoa mapema Leo

Mkuu wa makanisa ya Calvary Assemblies of God Mtume Dastan Maboya akiongoza Maombi ya kuwaombea viongozi kuanzia ngazi ya zote wa Taifa la Tanzania mapema leo Jijini Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...