Mhandisi. Joyce Kisamo akiwa mwenyefuraha baada ya kukabidhiwa TUZO ya LUCE ya mwanamke aliyefanya vizuri katika nishati, mazingira na sekta endelevu (Legacy Women Category).
 
🔴Ni  Tuzo ya kutambua mchango wa mwanamke aliyefanya vizuri katika nishati, mazingira na sekta endelevu
Ni tu
 
Na. Mwandishi wetu
Mtanzania Mha. Joyce Kisamo kutoka Wizara ya Nishati amekua muafrika wa pili kutwaa tuzo ya LUCE ya mwanamke aliyefanya vizuri katika nishati, mazingira na sekta endelevu.
 
Mnigeria Onyinye Anene-Nzelu ambaye ni Mkuu wa Gridi Ndogo katika Ufikiaji wa Nishati nchini Nigeria, aliwahi kunyakua Tuzo katika kundi la wanawake chipukizi 2023.
 
Joyce, ambaye ni Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati alibuka mshindi wa shindano hilo la Tuzo za LUCE katika kundi la Mwanamke mwenye uzoefu na aliyeacha alama na kuwashinda wanawake wengine 15 kutoka mataifa mbalimbali ya Ulaya na Asia.
 
Zaidi ya kura 2,000 zilipigwa duniani kote na kura 600 zilitosha kumpa ushindi Mha. Joyce ambaye alikuwa mwafrika pekee na katika kinyang’anyiro hicho ameibuka mshindi kwa kuacha alama nyingi katika utendaji wake wa kazi (Legacy Women Category).
 
Kwa ushindi huo Joyce ametambulika kimataifa kuwa Mwanamke mwenye uzoefu, aliyefanyakazi na kuacha alama zenye manufaa kiuchumi, kimazingira na kijamii katika Sekta Endelevu hususani Nishati Safi na Endelevu.
 
Makabidhiano ya tuzo hiyo yamefanyika leo tarehe 16 Mei,2024 huko Florence nchini Italy kisha mshindi atahudhuria Mkutano wa masuala ya Nishati Safi na Endelevu. (Flagship Conference) kuanzia tarehe 23 hadi 25 Mei, 2024 katika European University Institute.
 
Tuzo za LUCE, zimefanyika kwa mara ya pili na linaandaliwa na mpango wa Lights on Women kwa ushirikiano na Landwärme na Edison, linalenga kutambua na kusherehekea mchango mkubwa wa wanawake.
 
Lengo la kuanzisha mashindano hayo ni kutetea majukumu muhimu ya wanawake kuelekea matumizi bora ya nishati endelevu.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...