Na. Freddy Maro Arusha.

Mei 21,2024.

Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso amemteua Bi Christine Mwakatobe kuwa mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha AWSA kuanzia tarehe 13 Mei 2024. Bi Mwakatobe kwa sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo Cha Kimataifa cha Mikutano Arusha AICC.

Sehemu ya barua ya uteuzi inaaisha kuwa Waziri Aweso amemteua Bi Mwakatobe kwenye Bodi hiyo nafasi ya mwakilishi wa watumiaji wakubwa wa maji jijini Arusha.

“ Ni matarajio yangu kuwa utaupokea uteuzi na kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha iendelee kutoa huduma bora na zenye viwango vya hali ya juu,” Waziri Aweso alinukuliwa katika barua hiyo na kusisitiza kuwa Bi Mwakatobe atatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia miogozo na maelekezo ya Wizara ,Msajili wa Hazina na Serikali kwa ujumla.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa AICC mwezi Machi mwaka huu Bi Mwakatobe ambaye kitaaluma ni mchumi na mtaalamu wa masoko, alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji na Uendeshaji wa Kiwanja cha ndege cha Kilimanjaro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...