Kaimu Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akizungumza na wazazi, wanafunzi na viongozi na wadau wa elimu katika mkutano wa majumuisho mara baada ya washiriki wa juma la elimu kutembelea shule za msingi Mgusu na Mshikamano pamoja na Shule ya Sekondari Mgusu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita.

Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Geita, Bi. Linda Marandu akizungumza
na wazazi, wanafunzi na viongozi na wadau wa elimu katika mkutano wa majumuisho mara baada ya washiriki wa juma la elimu kutembelea shule za msingi Mgusu na Mshikamano pamoja na Shule ya Sekondari Mgusu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita.


Baadhi ya wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) na wadau wa elimu wanaoshiriki Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita wakiwa katika majadiliano na wanafunzi.

Afisa Elimu Watu Wazima Mkoa wa Geita, Bi. Salome Cherehani akizungumza na wazazi, wanafunzi na viongozi na wadau wa elimu katika mkutano wa majumuisho mara baada ya washiriki wa juma la elimu kutembelea shule za msingi Mgusu na Mshikamano pamoja na Shule ya Sekondari Mgusu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita.

Baadhi ya wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) na wadau wa elimu wanaoshiriki Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita wakiwa katika majadiliano na wanafunzi.


Kaimu Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akisisitiza jambo alipokuwa kwenye mkutano na wazazi, wanafunzi na viongozi na wadau wa elimu katika mkutano wa majumuisho mara baada ya washiriki wa juma la elimu kutembelea shule za msingi Mgusu na Mshikamano pamoja na Shule ya Sekondari Mgusu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Juma la Elimu Kitaifa, ambaye pia ni Meneja Mawasiliano wa Shirika la Uwezo Tanzania, Bw. Greyson Mgoi (kulia) akizungumza kuwatambulisha wadau wa elimu walipotembelea baadhi ya shule ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yaliofanyika Mkoani Geita.

KAIMU Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala amewataka wazazi na walezi wa wanafunzi katika shule za msingi Mgusu na Mshikamano pamoja na Shule ya Sekondari Mgusu kuhakikisha wanafunzi katika shule hizo wanapata chakula wawapo shuleni.

Kauli hiyo, imetolewa leo mkoani Geita katika ziara ya wadau wa elimu wanaoshitiki Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita, walipokuwa wakizitembelea shule hizo na kuzungumza na wazazi, wanafunzi, walimu pamoja na viongozi na wadau wa elimu. 

Alisema haki ya mtoto kupata chakula ni ya msingi hivyo ni jukumu la wazazi na walezi kuhakikisha wanakula ili waweze kusoma vizuri na hata kufaulu katika masomo yao, kwani mtoto akiwa na njaa hawezi kusoma na kuelewa kwa urahisi anachofundishwa na walimu.

"Naomba sana wazazi na walezi tuhakikishe kwamba watoto wetu wanakula wakiwa shuleni kwani watoto hawa muda mwingi wanautumia wakiwa shuleni tukiwaacha watoto hawa wakakaa na njaa wakiwa shuleni tunatengeneza matatizo ya kiafya kwao kama vidonda vya tumbo naomba tuchangie ili tuwanusuru," alisema Kaimu Mratibu wa TEN/MET, Bi. Makala akizungumza.

Aliongeza kuwa kiasi kinachotakiwa kuchangiwa kwa kila mzazi ni kilo moja ya mahindi na shilingi mia tano (500) tu kwa mwezi kiwango ambacho kinaweza kuchangiwa kwa kila mzazi kama amedhamiria kufanya hivyo. Kuna watoto 687 wanashinda na njaa kila siku wawapo shuleni huku wenzao 813 wanapata huduma ya uji shuleni kila siku. 

"...Ni vizuri mtoto asome akiwa ameshiba hapa anaweza kumsikiliza mwalimu vizuri, lakini tumboni akiwa hana kitu hawezi kumsikiliza mwalimu na kuelewa kirahisi...kwa hili nawasihi wazazi tusaidiane, Serikali inajitahidi kufanya kwa sehemu yake lakini wazazi na wadau wengine tuna kila sababu ya kuunga mkono juhudi hizo za Serikali"

Aidha aliongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, walimu na viongozi wa elimu ndio njia pekee inayoweza kuchochea maendeleo ya elimu katika eneo hilo. 

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Geita, Bi. Linda Marandu alisema licha ya uwepo wa changamoto hiyo ya baadhi ya wazazi kutoitikia uchangiaji wa chakula eneo hilo, lakini bado Kata ya Mgusu inaongoza kufanya vizuri katika uchangiaji chakula ukilinganisha na kata zingine eneo hilo. 

Baadhi ya walimu wakizungumza na wadau wa elimu walipofanya ziara katika shule hizo.

Baadhi ya wazazi na wanafunzi wakiwa katika vikao na wadau wa elimu.

Baadhi ya wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) na wadau wa elimu wanaoshiriki Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita wakiwa katika majadiliano na walimu.

Baadhi ya wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) na wadau wa elimu wanaoshiriki Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanayoendelea mkoani Geita wakiwa katika majadiliano na wanafunzi wa shule za msingi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...