Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde ameainisha mpango wa serikali wa kusaidia utatuzi wa changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo nchini.

Mh Mavunde ameyasema hayo leo wakati akijibi swali la Mh Dkt. Christine Gabriel Ishengoma Mbunge wa Viti Maalum aliyetaka kujua mpango wa serikali kuwasaidia Wachimbaji Wadogo wa Madini Wilaya ya Ulanga.

Akijibu awali hilo Waziri Mavunde amesema Mpango wa Serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo nchini wakiwemo wachimbaji wa madini wa Wilaya ya Ulanga unahusisha mambo yafuatayo:-

(i) Kuwekeza zaidi katika utafiti wa kina kugundua uwepo wa madini katika maeneo mbalimbali ili kuwaongoza vizuri wachimbaji wadogo;

(ii) Utoaji wa Leseni za uchimbaji kwa wachimbaji wadogo;

(iii) Kutoa Elimu ya matumzi ya teknolojia sahihi ya uchimbaji ili kuongeza tija;

(iv) Huduma ya uchorongaji kwa gharama nafuu kupitia Shirika la Madini Tanzania (STAMICO);

(v) Upatikanaji wa mikopo nafuu kwa wachimbaji kupitia Benki mbalimbali na Taasisi za fedha.

(vi) Fursa ya ukodishaji wa mitambo na vifaa chini ya usimamizi wa STAMICO kupitia makampuni yaliyoingia makubaliano(MoU) na STAMICO.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...