Ukarabati wa Kivuko cha Mv. Magogoni unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Mwezi Desemba, 2024 na kurejeshwa Nchini ili kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya Bungeni jijini Dodoma leo tarehe 30 Mei 2024 wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni Dkt. Faustine Ndungulile aliyeuliza ni lini matengenezo ya Pantoni ya Mv. Magogoni iliyopo nje ya Nchi yatakamilika na kurejeshwa nchini ili ianze kutoa huduma kwa wananchi.

Itaumbukwa kuwa Mwezi Februari 2023 Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) ilisaini mkataba wa ukarabati wa kivuko cha MV. MAGOGONI wenye thamani ya Shilingi Bilioni 7.5.

Lengo la ukarabati huo wa Kivuko cha MV. MAGOGONI ni juhudi na mikakati ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha miundombinu mbalimbali ya usafirishaji nchini, kuharakisha na kurahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa wananchi waishio katika Wilaya ya Kigamboni, Ilala na maeneo mengine.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...