Na WAF – Dodoma

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) kushirikiana na Wabunge kusambaza vifaa tiba ikiwemo vitanda vya kujifungulia katika majimbo yote 214 ya Tanzania Bara.

Waziri Ummy ametoa maelekezo hayo kwa MSD leo Juni 10, 2024 Bungeni Jijini Dodoma mara baada ya kujibu maswali ya Wabunge ambapo pia Mwenyekiti wa Bunge Dkt. Joseph Mhagama alihoji juu ya changamoto ya utekelezaji wa maagizo na maelekezo ya Viongozi wa Serikali kupitia watendaji.

“Katika mwaka wa fedha huu ambao tunakaribia kuumaliza, tumesambaza vitanda vya kujifungulia katika majimbo yote 214 ya Tanzania Bara, nilitoa maelekezo kwa MSD kuwa vitanda hivi vikakabidhiwe kwa Wabunge ili wao waweze kuvipeleka katika Hospitali na Vituo mbalimbali” amefafanua Waziri Ummy Mwalimu.

"Haya ni maelekezo ya Serikali yazingatiwe na sio tu vitanda vya kujifungulia ni pamoja na vitu vilivyonunuliwa na Serikali ikiwemo magodoro, Mashine za Ultrasound pamoja na X-Ray” amesisitiza Waziri Ummy.

Amesema kuwa Serikali inawajibika kwa wananchi kupitia kwa Wabunge hivyo ni lazima tuhakikishe ushiriki wa Wabunge katika masuala mbalimbali ya miradi inayotekelezwa na Serikali katika Sekta ya Afya.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...