Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati kwa udhamani mkuu wa SUN KING, inawaalika Wananchi wote katika Maonesho ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu (Renewable Energy)  yatakayofunguliwa Alhamisi Juni 6 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri Nishati, Dk Doto Biteko na kufungwa na Waziri wa Kilimo, Husein Bashe Ijumaa, Juni 7, mwaka huu. 

Kaulimbiu ya Mwaka huu ni: NISHATI JADIDIFU KWA UCHUMI SHIRIKISHI NA WA KIJANI (RENEWABLE ENERGY FOR INCLUSIVE AND GREEN ECONOMY)

Wiki ya Nishati Jadidifu itakuwa na maonesho yanayohusisha Umeme wa Jua yaani Sola, Upepo, Joto-ardhi na majiko banifu sambamba na warsha yenye mada mbalimbali kuhusu nishati jadidifu. 

Wadau wa maendeleo, kampuni na taasisi binafsi na serikari watakuwa katika mabanda kutoa elimu na kuuza bidhaa mbalimbali za nishati jadidifu kutoka kwa wataalamu waliobebea.

Wadhamini wengine wa Maonesho hayo yatakayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Posta, Dar es Salaam ni Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU), Expertise France, Ensol, GOGLA, Tanesco, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), AECF na UNDP

HAKUNA KIINGILIO.

WOTE MNAKARIBISHWA.

Kwa taarifa zaidi piga 0765 098 462.


Tanzania Renewable Energy Association(TAREA)

Plot 1080, Mandela Road, Mabibo External,

Export  Processing Zone Authority

Shopping Arcade 17,

P.O. Box 32643,16106 Dar es Salaam, Tanzania.

Email address: info@tarea-tz.org

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...