Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph amesema kukamilika kwa asilimia 98 ya mradi mkubwa wa maji wa Nzuguni uliyogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4.3 na kuanza kutoa huduma kwa wananchi tangu Disemba 23, 2023 ni mafanikio yaliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na baadhi ya wananchi waliyojitolea maeneo yao ili mradi huo uweze kutekelezwa kwa manufaa ya wananchi wa Nzuguni.

Mhandisi Aron amewashukuru wananchi wa Nzuguni katika Mkutano wa Hadhara uliyoitishwa na Mbunge wa Jimbo wa Dodoma Mjini, Mhe. Antony Mavunde Julai 10, 2024 ukiwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Hata hivyo, Mhandisi Aron ameendelea kuwasisitiza wananchi wapatao 33 kati ya 58 ambao hawajajitokeza kutambuliwa kwa ajili ya kupata fidia za maeneo yao kujitokeza ili zoezi hilo likamilike kabla ya malipo ya fidia zao kuanza kulipwa.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Aron ameutambulisha Mradi wa kusaidia Kaya zisizo na uwezo kuunganishiwa huduma ya maji na DUWASA (WFL)kwa gharama nafuu ya shilingi Elfu Thelathini tu baada ya kufanyika utambuzi wa kaya hizo kwa ushirikiano na viongozi wa mitaa na kata katika Kata za Ntyuka(Chimala), Ndachi na Nzuguni (Nzuguni A) utakaoanza mwezi Agosti, 2024 ambao unagharimu kiasi cha shilingi Milioni 970.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...