Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania(TET) Dkt. Aneth Komba ametoa rai kwa wadau mbalimbali wa elimu nchini kutembelea katika katika maonesho ya kibiashara ya kimataifa ya Dar es salaam hususani katika banda la TET ili kuweza kufahamu utekelezaji wa Mtaala ulioboreshwa.

Ameyasema hayo leo Julai 9, 2024 wakati aliopotembelea katika maonesho hayo katika viwanja vya sabasaba jijini Dar ea salaam ambapo ameeleza kuwa TET imeendelea kutoa elimu kwa wadau nchini kwa kuwaelewesha maboresho ya Mitaala yaliyofanyika, ambayo utekelezaji wake ulianza mwezi Januari 2024.

"Wadau tembeleeni katika banda letu hapa mtapata kufahamu masuala mengi kuhusiana na utekelezaji wa Mitaala iliyoboreshwa." amesema Dkt.Komba.

Pia, amesema kuwa TET inaendelea na uuzaji wa vitabu vya kiada kwenye maonesho hayo, hivyo kuwakaribisha wananchi wanaohitaji vitabu vya kiada vya Mitaala yote.

Katika ziara hiyo, Dkt.Komba alipata pia nafasi ya kutembelea katika mabanda mengine yakiwemo NECTA, NACTVET NA TBC.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...