Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Stanslaus Nyongo (Mb.) amesema Maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara maarufu (Sabasaba) ni fursa muhimu ya kutangaza na kuwakaribisha wawekezaji ili kuona fursa mbalimbali za uwekezaji nchini.

Ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2024 katika mahojiano maalumu aliyofanya baada ya kutembelea Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji zilizoshiriki maonesho ya Sabasaba.

Ameongeza kuwa Maonesho hayo yamekuwa na mvuto mkubwa kwa kuwa Wizara na Taasisi zilizoshiriki zimeonesha fursa zilizopo katika uwekezaji.

"Tanzania tunaona hii ni fursa nzuri ya kujitangaza kama nchi na kukaribisha wawekezaji mbalimbali kuona fursa za uwekezaji katika nchi yetu" amesema Mhe.Nyongo

Aidha, amepongeza namna ambavyo wafanyabishara wamekuwa wabunifu na makampuni ya nje yaliyokuja kuonesha shughuli za uwekezaji wanazoweza kufanya nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...