Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Stanslaus Nyongo (Mb.) amesema Maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara maarufu (Sabasaba) ni fursa muhimu ya kutangaza na kuwakaribisha wawekezaji ili kuona fursa mbalimbali za uwekezaji nchini.
Ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2024 katika mahojiano maalumu aliyofanya baada ya kutembelea Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji zilizoshiriki maonesho ya Sabasaba.
Ameongeza kuwa Maonesho hayo yamekuwa na mvuto mkubwa kwa kuwa Wizara na Taasisi zilizoshiriki zimeonesha fursa zilizopo katika uwekezaji.
"Tanzania tunaona hii ni fursa nzuri ya kujitangaza kama nchi na kukaribisha wawekezaji mbalimbali kuona fursa za uwekezaji katika nchi yetu" amesema Mhe.Nyongo
Aidha, amepongeza namna ambavyo wafanyabishara wamekuwa wabunifu na makampuni ya nje yaliyokuja kuonesha shughuli za uwekezaji wanazoweza kufanya nchini.


Ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2024 katika mahojiano maalumu aliyofanya baada ya kutembelea Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji zilizoshiriki maonesho ya Sabasaba.
Ameongeza kuwa Maonesho hayo yamekuwa na mvuto mkubwa kwa kuwa Wizara na Taasisi zilizoshiriki zimeonesha fursa zilizopo katika uwekezaji.
"Tanzania tunaona hii ni fursa nzuri ya kujitangaza kama nchi na kukaribisha wawekezaji mbalimbali kuona fursa za uwekezaji katika nchi yetu" amesema Mhe.Nyongo
Aidha, amepongeza namna ambavyo wafanyabishara wamekuwa wabunifu na makampuni ya nje yaliyokuja kuonesha shughuli za uwekezaji wanazoweza kufanya nchini.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...